GivePower Yashinda Tuzo Kuu Kimataifa kwa Teknolojia Yake ya Ubunifu ya Shamba la Maji Linalotumia Nishati ya Jua.
Teknolojia ya kuondoa chumvi majini inayotumia nishati ya jua yashinda tuzo ya nafasi ya kwanza katika hafla ya Dubai iliyolenga suluhisho za mgogoro wa maji duniani.
DUBAI, Falme za Kiarabu, Feb. 05, 2020 (GLOBE NEWSWIRE) — GivePower ilitwaa heshima kuu katika jukwaa la kimataifa, ikipokea Tuzo ya Kimataifa ya Maji ya Mohammed bin Rashid Al Maktoum kwa teknolojia yake ya Solar Water Farm. Tuzo hiyo ilizinduliwa na Mheshimiwa Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Mtawala wa Dubai, ili kuhimiza taasisi za utafiti, watu binafsi, na wabunifu kutoka kote ulimwenguni kubuni suluhisho endelevu na bunifu kwa uhaba wa maji yanayotumia nishati ya jua. Taasisi ya UAE Water Aid Foundation, Suqia, ndiyo inayosimamia tuzo hiyo, ambayo ina makundi makuu matatu: Tuzo ya Miradi ya Ubunifu, Tuzo ya Utafiti na Maendeleo ya Ubunifu, na Tuzo ya Mtu Binafsi wa Ubunifu. GivePower ilishika nafasi ya kwanza kwa Tuzo ya Miradi Midogo ya Ubunifu.
Kwa Mwanzilishi, Mwenyekiti, na Mkurugenzi Mtendaji Hayes Barnard, aliyekubali tuzo hii mjini Dubai kwa niaba ya GivePower, shirika lisilo la faida la Marekani lenye hadhi ya 501(c)(3), tuzo hii inawakilisha uelewa unaokua kuhusu mgogoro wa maji duniani kote, na msaada unaohitajika ili kuunda suluhisho bunifu zinazoweza kuokoa maisha. Kwa msaada na uungwaji mkono wa Taasisi ya UAE Water Aid, GivePower itaweza kuendelea kusambaza Mashamba ya Maji ya Jua kwa watu wanaohitaji sana kupata maji safi ya kunywa. [Soma Makala Kamili]